SOMO:NAMNA YA KUOMBEA HALI YA KIROHO YA ARDHI ILI UFANIKIWE KIMAISHA. (4&5)

SOMO:NAMNA YA KUOMBEA HALI YA KIROHO YA ARDHI ILI UFANIKIWE KIMAISHA. (4&5)

4. SIKU YA NNE YA SEMINA YA NENO LA MUNGU-IRINGA NA MWL CHRISTOPHER MWAKASEGE(MANA MINISTRY)

LENGO:Kujifunza mbinu za kuomba ili hali ya kiroho ya ardhi iliyokwamisha mafanikio yako iondoke ili uweze fanikiwa.

HATUA ZA KUMSAIDIA MTU ILI AONDOKE AU WEWE UONDOKE KATIKA HALI HIYO ILIYOKWAMISHA KUANZA UJENZI,KUENDELEA AU KUMALIZIA UJENZI..

5.MUULIZE ALYEHITAJI KUOMBEWA IKIWA AMEWAHI KUTAFUTA KUPATANISHWA KIROHO AU KUFUATA MASHARTI YALIYOPO KTK ARDHI ANAYOJENGA AU ALIYOKWISHA JENGA.

2FALME 17″24-29.

Ile kwamba mwenye kiwanja amekuuzia haina maana mungu wake ameondoka pia.Unapohamia mahali hapo au kujenga hapounakutana  na masharti tofauti na mungu wako , ni lazima ufuate masharti ya pale ili uweze kukaakwa AMANI.

Unafika eneo la kazi wanakwambia ni lazima upatane ana mungu wa pale ili ufanye kazi kwa amani.Unaweka hirizi au unasimika nyumba kwa mizimu ya mababukwababu unaamini kwa miungu ile ina umuliki wa ardhi,kumbuka Mungu ana wivu na palipo na wivu pana ugomvi, kwa hiyo Mungu hataki mtu anaye changanya mambo,hirizi penye kujenga halafu unaenda kumwomba Mungu kanisani-unaleta matatizo.Inawezekana unakabidhiwa mahali hapo haujui kuwa mahali hapo watu walikabidhi kwa miungu wao.

6.OMBA TOBA KWA MUNGU KWA AJILI YA MAENEO YAFUATAYO:

A.Kwa kuvunja kwa kutofuata masharti ya Mungu yanayohusu ardhi inayotumika kujenga(kuchanganya miungu).Mungu alipokuwa ana waadhibu wana wa Israeli alikuwa hana shida na watu bali madhabahu ya miungu mingine.
B.Omba toba kwa kilichosababisha shetani akapata nafasi ya kumiliki eneo na kupata nafasi.Shetani hakupewa nchi wala mbingu wala ardhi BALI nchi walipewa wanadamu.Danieli 9:16

Maombolezo 5:7.
Unatubu dhambi kwa ajili yako bali uovu kwa ajili ya babu zako.

MALAKI 1:3-4. MWANAZO 36:40-43.
Babu yake alipojenga pamebolewa,pakabolewa lakini ameshindwa kujenga mtoto anasema watajenga lakini Mungu anasema atabomoa.
Baba amekufa unataka kujenga hujajua nini kilichosababisha pakabomolewa unajenga!Mungu anabomoa,bila toba EDONI hawezi jenga, Mungu amezuia Edoni asijenge si kwa ajili ya uovu wa baba yake, bali uovu hutuwekea mipaka na babu zetu.

7.OMBA MUNGU AONDOE MAZINGIRA YA UKIWA ILI ZUIO LA KUJENGA LIONDOKE NA MADHARA YAKE KWAKO AU KWA HUYO UNAYEMUOMBEA, MADHARA YALIYOZUIA UJENZI.
EZEKIELI 35:9.

Ukiwa unaondoa watu kutokuishi au kujenga.
ISAYA 5:9.
Ukiwa unazuia mipaka na wapangaji na wenye eneo.Watu wanakuwa hawaji hata kupanga hapo au kujenga.
EZEKIELI 33:28.
2 SAMWELI.13:20
Ukiwa unakuhalalishia kukaa ndani hata kama unaweza fanya kazi.Ukiwa unazuia ujenzi.
AMOSI 6:11.YEREMIA 51:26,29 15:8.
Ukiwa unahalalisha nyumba kukomea kwenye misingi. UKIWA ni matokeo ya KUKOSA .
8.VUNJA NA ONDOA LAANA ILIYOPO KTK ARDHI YA ENEO LA UJENZI. YOSHUA 6:26.
Shughulika na laana iliyopo katika eneo hilo kwa Damu ya Yesu maana inasafisha kila kitu.
9.KEMEA ILI VIONDOKE VYOTE VILIVYOKAA KTK ENEO LOTE UNALOLIOMBEA LILILOSHINDIKANA KUJENGWA AU HALIKALIKI HATA BAADA YA UJENZI. ISAYA 13:19-22.

Ukiwa pia unapoteza wale waliobaki uwezo wa kufanya kazi kupotea.Nyumba zilizobaki tupu huwa makazi ya bundi,panya, majini na mapepo. Unaweza ukanunua gofu ukajua lipo tupu tu, au nyumba ukajua ipo tupu,au kiwanja na kama haujakemea vitu visivyo vya Mungu humo ndani vitakutesa sana, unapaswa kukemea viondke na uingie na DAMU YA YESU.

10.OMBA MUNGU AKUJULISHE IKIWA UKIWA UMEONDOLEWA NA WATU HAO WABAYA..

UKIWA ni ZUIO linalotumika kuzuia kitu flani kwa ajili ya mtu yule aliyewekewa kutengeneza EZEKIELI 45:1-4, 48:8-9.

Kuna majengo mengi yamekwama kwasababu yamewekewa ZUIO,kama Mtumishi wa Mungu unatakiwa uondoe zuio hilo.

YEREMIA 4:27-28. ISAYA 6:1-4.
Roho Mtakatifu akishuka atakupa FURAHA badala ya MAOMBOLEZO.Watu wengi wana magari lakini hawana nyumba kwasababu ya zuio ktk ulimwengu wa roho kuwa na UKIWA washindwe kujenga,
11.WEKA WAKAFU KWA MUNGU HILO ENEO.
MkabidhiMungu hilo eneo, inawezekana Mungu amekupa eneo lakini anataka umkabidhi kwake rasmi.Ukilishikilia na kulimiliki eneo hilo kwa Damu ya Yesu Mungu anakupa plan ya hilo eneo.Weka wakfu ardhi,mipaka,misingi,malango na ramani ya kiwanja.
Mungu hukupa vipimo, vitakuwa vyumba vya watoto wangapi, wageni wa namna gani?.Mungu akupe cha kwako usiige cha wengine bali pata cha Mungu maana ana plan ya maisha yako ya baadaye.Weka wakfu kwa kila kitu maana kwenye ramani zingine kuna vitu visvyo vya Mungu pia.

12. VISEMESHE ARDHI NA MBINGU VISIKWAMISHE UENDELEZAJI WA UJENZI NA UTUMIAJI WA KITAKACHOJENGWA.KUMBUKUMBU LA TORATI 32:1.

Ni vizuri kuitangazia ardhi kilichoondoka na Mungu amenipa eneo hili ili usikwamishe.Ukishasemesha ardhi inasikia na mbingu inasikia. Neno linaposema mbingu iliwafunika maana yake ni kwa ajili ya watu wengi bali inaposema mbingu ikikufunikia ina maanisha ni kwa ajili ya mtu mmoja

5. SIKU YA TANO NA YA MWISHO

LENGO:Kujifunza mbinu za kuomba ili hali ya kiroho ya ardhi iliyokwamisha mafanikio yako iondoke ili uweze fanikiwa.

MBINU ZA KUOMBA ILI KUWAFUNGUA WALIOFUNGWA NA JELA YA KIROHO YA ARDHI Matendo 16:26.

Tunajifunza Paulo alikemea lile pepo lakini kumbe ulikuwa mradi wa watu wa pepo wa uaguzi,unaweza ukawa unafanya vitu kumbe watu wengine ni mradi wao na ukaanza kuapata vita toka kwao(waganga)
Paulo alipofanya maombi kule gerezani tetemeko halikutetemesha gereza tu bali MISINGI ya gereza ilitikisika na milango ikafunguka.
Mstari 26-milango ya gereza ilifunguliwa kabla vifungo havijalegezwa, vigungo hulegezwa na matokeo ya msingi na milango kulegezwa.
Ile nguvu ilienda kwenye misingi ya KIROHO  iliyofunga akina Paulo wasiendelee kwa jinsi ya mwili pia.Jinsi ya kiroho  haimtishi shetani bali misingi ya kiroho, tunatembelea madaha kwa Kristo kwasababu tumekombolewa KIHALALI kwa Damu yake.Ni Lazima kuombea misingi ya kroho ya mahali hapo ili milango ya mafanikio ifunguke na iachie.
MAOMBOLEZO 3:33-35.
Inaonyesha watu wote walifungwa kwenye ardhi,unaweza kuwa unatembea kwa madaha uko huru  mtaani lakini kumbe kiroho ni mfungwa wa ardhi hiyo na hufanikiwi.
Kumbukumbu la Torati 6:12 7:8
Nchi inaweza kuwa imewekewa utumwa kwenye ardhi lakini watu wakawa wanaishi hivyo wakifikiri wapo huru kumbe kuna mahali wamefungwa wasiendelee.
ISAYA 14:24-27.
Ukikanyaga ardhi  kwa mamlaka aliyokupa Mungu ndipo NIRA yako itakapoondoka kwa kifungo kilichokufunga. Ukikanyaga juu ya ardhi ile nira itaondoka  na kubatilisha ardhi ktk ulimwengu wa kiroho.
KIFUNGO CHA KIAPO KATIKA ARDHI.
WAEBRANIA 3:14-19 HESABU 14:22-45.
Neno la Mungu linaposema “KAMA NIISHIVYO” maana yake ni KIAPO CHA MUNGU.
Mungu alifunga kiapo kwa wana wa Israeli jangwani walishindwa fanikiwa kwasababu ya uasi,
HESABU 30:2, 12-16.
Kiapo ni kifungo cha kiroho.Nafsi inabeba hisia,maamuzi,fikra, nia na makusudi ya mtu.
Ikiwa umefungwa katika kiapo flani NI LAZIMA ukibatilishe kile kiapo na UTENGUE.
EZEKIELI 21:18-23.
Kwenye mistari hii inaposema alipelekwa kwenye NJIAPANDA ili ale kiapo ,NJIAPANDA maana yake ni KUKOSA MAAMUZI, unakuwa njiapanda uolewe au usiolewe,usome au usisome,ujenge au usijenge,ufanye huduma ya Mungu au kazi nyingine,biashara au siasa n.k UPO NJIAPANDA.
Unaweza ukaota ndoto vitu vikatokea ndotoni -ardhi imefungwa ufeli,inakufunga usifanikiwe kwa njia za KI-MUNGU kabisa bali ufanikiwe kwa njia za ki-miungu hiyo unakuwa umefungwa usipotangua itakutesa.
Mji wa Yeriko ulikuwa umefungwa jela ya kiroho ya ardhi.Mungu alipokuwa amepeleka watumishi wake alikuwa hana shida na Yeriko bali shida yake ilikuwa kwa Rahabu ktk ukoo wa Yesse kwasababu ardhi ilimfunga.
Watakuja wahubiri atahubiri watu hutapona kumbe tatizo liko kwenye ardhi ambayo ndiyo imekufunga katika tatizo hilo.
Punda wa Yesu alikuwa amefungwa kinabii kwa ajili ya BWANA YESU na hakuna aliyemtumia mpaka Yesu alipokuja.Unaweza pia nawe katika familia,ukoo,jamii, au taifa lako umekuwa punda uliyenenewa na mababu zako imefika kipindi chako cha ujana ustawi unashindwa! kwasababu umefungwa ktk kiapo flani katika familia au ukoo hausogei ktk Elimu, au biashara, au kiuongozi, ndoa,kiuchumi,kiroho,,kujenga,au n.k.PUNDA UMEFUNGWA.

Na ivyo hivyo Mungu alisema  kwa ajili ya maisha yako atafanya CHAKE.imefika unataka ufanye kingine unachotaka wewe HAKITAENDA bali BWANA atafanya chake kwasababu BWANA anasema ana haja nawe, utafanikiwa na kustawi ni kwasababu  cha BWANA( kwasababu maisha yako yamefungwa kumtumikia Mungu)

Ni lazima ukae kwenye LANGO kwasababu Mungu anataka kukupitisha  ili kufungua milango ya mafanikio yako ili ufike kule BWANA alipoweka KUSUDI LAKE na kwa KIWANGO CHAKE sio viwango vya wanadamu.

ILI KUFUNGULIWA TOBA NI MUHIMU kwasababu 1.Mungu anakusamehe na 2.Mungu atakurehemu na DAMU YA YESU itasema maneno mazuri juu yako, UTAMILIKI juu ya VYOTE  na ROHO WA BWANA atakuwa Juu yako.
Mwisho wa Semina hii, tutendee kazi haya tutafanikiwa,tusiwe wasikilizaji tu.

HAKIKA TUTABARIKIWA NA KULA MEMA YA NCHI.



Reactions

Post a Comment

0 Comments