SADAKA

MJUE MUNGU ILI UWE NA AMANI | IJUE BIBLIA


SOMO: SADAKA

UTOAJI KAMA MUALIKO WAKO BINAFSI KUTOKA KWA MUNGU



Kumbukumbu 12:10-11,13-14

13- Ujihadhali usitoe sadaka kila mahali upaonapo/upapendapo (anywhere you please)

Ndugu hatuna amri/ ruhusa/machaguo (choice) ya kutoa sadaka popote tupendapo sisi

5 – Lakini mahali atakapopachagua BWANA, Mungu wenu (you are to seek the place the LORD, your God will choose….)

 14- Bali katika mahali alipopachagua BWANA, …..na kutenda yote nikuamruyo  

-          Kutoa kwa Imani ni kutoa kulingana na maelekezo amabyo umepewa na BWANA na sio ya kwako ama upendavyo wewe kutoa sadaka.

-          Mungu anaposema jihadhali maana yake kuna watu wengi wanapuuzia na kutoa sadaka kama wapendavyo wao wenyewe ama viongozi wao.

-          Usitoe kwa sababu watu wana shida , huo ni msaada na sio sadaka, Usitoe msaada ukaita ni sadaka.

-          Sadaka hutolewa kwa maelekezo toka (instructions) to kwa Mungu mwenyewe unayemtolea, hata kwa waganga wa kienyeji hamtoi kile mpendacho bali kile waamurucho kutoa, Je si zaidi sana kwa Mungu kutoa atuamurucho kutoa.

Je, Utajuaje kwamba hapo unapotolea sadaka ndipo BWANA alipopachagua?

JIBU: Ni pale tu alipoamua kulikalisha jina lake ( alipoamua kuwepo sehemu hiyo); na sio mahali pa kuliitia jina lake.

Kumb: Jifunze kutofautisha mahali alipoliweka jina lake na mahali pa kuliitia jina lake.

Mathayo 18: 20

 Walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao/ Pamoja nao

 Key point | Wamekusanyika kwa jina langu – alipochagua kuliweka jina lake

Sio popote mkusanyikapo nyie jina lake linakuja, hapana mnapaswa kufuata mahali alipoliweka jina lake, na ndio maana hema au hekalu halikujengwa popote ili watu wawili watatu wakusanyike, walijenga alipochagua BWANA kukaa mahali hapo uwepo wa Mungu unakuwepo.

-          Usitoe Sadaka sehemu ambapo jina lake halipo / uwepo wake  haupo

-          Biblia haimuruhu mhubiri au mchungaji au askofu yeyote kuelekeza (Dikteti/Amuru) sehemu ya kutolea sadaka.

-          Biblia pia haimpi ruhusa mtoaji sadaka kuamua /kudikteti mahali pakutolea sadaka au namna ya kuitoa sadaka hiyo.

-          Biblia inasema usitoe  mahali popote bali BWANA atakapo pachagua na kuamua kulikalisha jina lake

-          Lolote tulifanyalo tulifanye kwa jina lake, kumbuka kulitaja jina lake tu hakufanyi pepo litoke maana kuna hata wanadamu wanaitwa majina wa kina yesu, Shetani ( Mapepo Jeshi) haogopi jina la Yesu anaogopa uwepo (presence ) wa mwenye jina

-          Wanafunzi wa Yesu walipoulizwa kwa mamlaka/ amri ya nani ? na kwa jina la nani ? mna fanya haya

Wakajibu;

                 Kwa jina la Yesu wa Nazareti, mlie Msurubisha

 

-          Unapotoa sadaka toa mahali ambapo jina lake limekaa hapo, maana yake palipo na uwepo wake mwenye jina.

Mathayo 6: 26- Hazina ya mtu ilipo, ndipo na moyo wake utakapo kuwa

 Kwa kawaida tu mali zako zilipokaa ndipo mawazo yako na akili yako yote ipawazapo na kupafikiria wakati wote.

-          MUNGU anapotaka ulete sadaka yako anataka akutane na moyo wako,

-          Kwahio basi, Unapotoa sadaka, tarajia kukutana na Mungu pale unapopeleka sadak

-          Mungu akisema peleka sadaka kanisani atakupa na kanisa specific, sio uchague wewe kanisa kwa sababu umeambiwa kupeleka kanisani.

-          Imani huja kwa kusikia ila si mkila anayesikia huwa na Imani maana kama ni hivyo ulimwengu mzima umesikia mahubiri toka kwa watu mbalimbali.

-          Imani huja kwa kusikia Neno la Mungu, Ila Ili Neno liwe Imani lazima libadilike kuwa personal instructions ( maelekezo binafsi ), Neno lisipokusukuma kuchukua hatua/matendo (kufanya/kuacha) halijawa Imani hata usikie mara milioni.

-          Neno la Mungu likikwambia nenda mahali Fulani kanitolee sadaka mahali hapo lazima ukifika utakuta uwepo wake hapo.

Soma Mwanzo 28: 10-22 Utakuta Habari ya Yakobo na uwepo wa Mungu alipolala mahli pale Yakobo alifanya Nyumba ya Mungu.

Kama unauhakika (Imani) ya kuwa Mungu ndiye aliyekuelekeza kutoa sadaka mahali alipokuelekeza kutoa sadaka na ukafika hapo ukakuta uwepo wake haujajidhihirisha utafanya nini?

-          Kumbuka, Mungu amekutuma uwende kukutana naye sio kutoa sadaka tu ( maana kama fedha-dhahabu na mali zote ni zake, kama ni kondoo Wanyama wote wa kondeni/mbugani ni wake akitaka anajitwalia)-mkumbuke Ibrahimu alibalikiwa kwa kukutana Mungu pa kutolea sadaka.

-          Usitolee sadaka na kuondoka kwa sababu amesema utoe sadaka mahali hapo, muombe Mungu ajidhihirishe mahali hapo huo ni uhuru wako kufanya hivyo

Mwanzo 22;1

kumbuka Ibrahimu alipokuwa akiaandaa pa kutolea sadaka Mungu hakujidhihirisha mpaka alipotaka kutoa sadaka. Kumbuka pia Mungu huchagua aina ya sadaka anayotaka umtolee sio unayotaka wewe.

-          Watumishi wa Mungu hawawezi kurudisha heshima ya Mungu, bali Mungu mwenyewe, hivyo hawawezi kumtengenezea Mungu pa kutolea au kumchagulia aina ya sadaka ya kumtolea.

-          SOMA Habari ya Gideoni kwenye kitabu cha waamuzi 6; 11-24

Gideoni alimjengea Mungu Madhabahu mahali pale alipomuona malaika wa Bwana.

Ndio maana Mungu anasema Beware/Jihadhalini

Kuna Nguvu za Mungu zinakuwepo mahali halafu zinanyamaza, unatakiwa kuzi activate/ kuziamsha/kuzifanya zifanye kazi, watu wengi huridhika wakikutana na wahubiri wakombewa matatizo yao, wanasahau kuwa aliyewaita kwenda kumtolea sadaka sio muhubiri bali ni Mungu kabla hawajakutana na Mungu wao wanarudi nyumbani wanaziacha sadaka zao, ndio maana matatizo yao hayaishi kwani wahaubir ni saw ana mtu kuumwa malaria halafu akanywa dawa za kutuliza maumivu . hamtibu magonjwa yenu badala yake mnapata relief ( tumaini/faraja) utapona endelea kuamini mpendwa, wao sio Mungu hakikisha umeuona uwepo wa Mungu ndio utoe sadaka.

Kutoka 25; 1-3,8

1-3- Wanitwalie sadaka; kila mtu ambaye moyo wake wampa kupenda…sadaka utakayo pokea mikononi mwao ni hii…..

8- Nao wanifaniyie patakatifu, nipate kukaa katikati yao

Unaona hapo juu anasema ambayo moyo wako utapenda kutoa, lakini chini anasema sadaka utakayo toa ni ipi, unaweza moyo wako ukapenda kutoa gari lakini Mungu akataka kuku, kuwa makini mpendwa sadaka hutolewa na huagizwa kutolewa kwa malengo maalumu.

Swali ni je sadaka tunayotoa kila siku za jumapili huwa ni ya nini/lengo lipi ?

Na ndo maana huwa tunatoa chochote..tunatoa bila malengo/ makusudio…

-          Alipokuwa anaagiza sadaka alikuwa anataka nini?

-          Ili wamfanyie patakatifu, ili akae kati yao

-          Usitafute motive yako( usisukumwe na hali yako/au mawazo yako) au ya muhubiri tafuta motive ya Mungu kwenye kutoa sadaka, na motive ya Mungu ilikuwa kukaa kati yaw ana Israel ili kukaa nao ilibidi watoe sadaka ili wajenge patakatifu.

-          Hema/Kanisa sio sehemu ya ibada au ofisi ya Haruni/Mhubiri (ni Dwelling place-masikaniya  Mungu na wanadamu-pa kukutana na Mungu physical-katika mwili)

Kutoka 29; 10,42-46

10- ….mbele ya hema ya kukutania

42- …..hema ya kukutania mbele za BWANA, hapo nitakapokutana nanyi , ili ninene nawe hapo

43- ….nami nitakutana na wana Israel mahali hapo , .. hema itafanywa takatifu kwa utukufu wangu

45- ..nami nitakaa kati ya wana Israel, nami nitakuwa Mungu wao

 

-          Utukufu- ni uwepo wa Mungu kuonekana katika mwili mbele za wanadamu (physical presence of God)-( Neno kufanyika mwili-Yohana 1; 1-10)

-          Ili uwe na Imani lazima Neno lifanyike kuwa mwili; lazima uone tofauti katika mwili-kungaa kwa sura ya Musa baada ya kukutana na Mungu

Hivyo mpendwa sadaka ni njia Mungu huitumia kukutana watu wake na sadaka hufanya Mungu akae na watu wake hivyo hakikisha unapeleka sadaka yako alipoliweka bwana jina lake na uwepo wake upo mahali hapo uwepo ambao ukikutana nao utaona tofauti katika mwaili wako..kama aliuona Musa, tusitoe sadaka kwa mazoea kwa sababu wachungaji wamesema tumtolee Mungu bali Mungu mwenyewe akwambie umtolee..mengine yote tuyafanyayo sio sadaka bali ni michango tu kama michango ya misiba, harusi na mingineyo..kama unatoa mali zako kwa sababu umetaka wewe au umeagizwa na mchungaji hiyo sio sadaka..ni mchango yu ..unpotoa pesa kuchangia ujenzi wa kanisa hiyo sio sadaka mpaka Mungu mwenyewe amekwambia moyoni mwako..kama sivyo itakuwa ni mchango kama michango mingine..

Unasema naongea nini unamiaka mingapi toka umekuwa ukitoa sadaka kanisani ..ni sadaka ngapi umetoa bila kuona tofauti na ngapi ulipotoa kuna kitu Mungu amekufanyia katika maisha yako.

Sadaka ambazo hazikuleta mabadiliko kwako hizo zote ni michango sio sadaka, bali sadaka ni zile ambazo ulipotoa zilikukutanisha na Mungu wako akafanya kitu kwenye Maisha yako..na macho yako yakawa shuhuda wa hayo.

 

Kumbukumbu 12;13

Jihadahalini usitoe sadaka kila mahali upaonapo

 

Mungu akubariki san ana akupe kufuliwa macho ya rohoni yakamuone, na masikio yako yakapate kusikia sauti yake ili upone.

 

By. Emmanuel M. Mhombwe                                                                 +255763786083


Reactions

Post a Comment

0 Comments